Freemason
Imekuwa Ikitajwa kwenye kila aina ya minong’ono. Tumeona matangazo
yakialika watu kujiunga nao kama wanataka kupata utajiri na kuwa watu
wenye nguvu. Lakini bado Freemason, imebaki kuwa kitendawili miongoni
mwa Watanzania wengi.Leo
tunakuletea habari kuhusu Mtanzania maarufu aliyefungua kinywa na
kueleza namna alivyojiunga na Freemasons, kundi lililo kongwe duniani.
Tayari
watu mbalimbali watu wenye hamu ya kupata utajiri wamekuwa wakitoa
ushuhuda kuhusu kundi hilo na kusikika kwenye vyombo vya habari, hasa
baada ya kifo cha mwingizaji nyota, Stephen Kanumba, mwaka 2012.
Siyo
hivyo tu, bali kumeibuka pia matangazo yenye namba za simu
yanayoshuhudiwa kwenye nguzo za simu mitaani hadi vichochoroni
yakiwataka watu wanaotaka kujiunga na Freemason kupiga simu ili wapewe
utaratibu wa namna ya kujiunga kwenye ‘kisima hicho cha mafanikio’.
Baadhi
ya watu tayari wameshanaswa na mtego huo, huku wengine wakiendelea
kujaribu bahati yao kujipatia utajiri kwa njia ya ‘nguvu za giza’.
Hata
hivyo Jayantilal Keshavji Chande, maarufu zaidi nchini kwa jina Sir
Andy Chande, aliyejiunga na Freemason Oktoba 25, 1954 baada ya kupita
kwenye usaili mzito, anaeleza namna alivyoibuka kutoka familia ya
kawaida hadi kuwa kiongozi wa Freemason Afrika Mashariki.
Sir
Andy Chande, ambaye amekuwa mwanachama wa kundi hili kwa karibu miongo
sita sasa, anaeleza namna alivyosajiliwa na kufikia hatua ya juu ndani
ya kundi hilo.
Chande
alizaliwa Mombasa Kenya, Mei 7, 1928, ingawa wazazi wake walikuwa
wakiishi Bukene mjini, mkoani Tabora, magharibi mwa Tanzania.
Katika
kufafanua utaratibu mzima wa Freemason, Chande ameandika kitabu
alichokiita; ‘A night in Africa-a journey from Bukene’ (Usiku wa
Afrika-Safari kutoka Bukene), pengine akitaka kuweka sawa dhana na
kuondoa tofauti ili misingi inayoendesha Freemason ifahamike.
Imani
ya kimaadili na thamani ya kundi hilo ilianza wakati wa mazungumzo yake
na Messrs Campbell Ritchie na McLean mwanzoni mwa miaka ya 1950.
Nataka kujiunga na ichochama cha freemason namba yangu ni 0784017108
ReplyDelete